SANTHOME SABS GIRLS' SEC.

Image Image Image

Jinsi ya kujiunga na shule yetu

Tafadhali bofya hapa kusoma maelezo ya kina kabla ya kulipia fomu

Maelekezo ya kununua fomu mtandaoni

  1. Lipia TSh 25,000/= kwenye mojawapo ya namba zifuatazo
    0764 637 877 
    Jina: SANHTOME SABS GSS
    Tumia namba ya simu kufanya malipo. Usiweke pesa kwa wakala wala kuhamisha toka benki kuja kwetu moja kwa moja.
    Ukitumia wakala / benki hatutapata namba ya simu iliyofanya malipo hivyo mifumo yetu haitaweza kushughulikia muamala wako
  2. Ndani ya muda mfupi tutakutumia ujumbe kwenye namba uliyoitumia kufanya malipo. Ujumbe huo utakuwa na token.
  3. Bonyeza Pakua fomu. Ingiza namba ya simu uliyotumia kufanya malipo.
  4. Ingiza token tuliyokutumia kwa ujumbe mfupi
  5. Ingiza majina mawili ya mwanafunzi kwenye sehemu husika, kama alivyosajiliwa kwenye mtihani wa darasa la saba. Ingiza pia eneo anakotokea
  6. Ingiza jina la shule aliyomaliza darasa la saba. Kisha chagua kama ni English Medium au shule ya Kiswahili.
  7. Chagua tarehe atakayoweza kufika shuleni Dodoma saa mbili asubuhi kufanya interview kati ya siku tatu zilizoorodheshwa. Hakutakuwa na interview nyingine
  8. Hakiki taarifa hizi kwani hutaweza kubadilisha, kisha bonyeza Hifadhi Taarifa
  9. Pakua fomu. Ichape na ufuate maelekezo yake.
  10. Siku ya interview uliyochagua, uje na fomu original iliyoambatanishwa picha pamoja na vyeti vya mwanafunzi shuleni Dodoma.